Imefikia Wapi Kesi ya Aliyeandika Jenerali MWAMUNYANGE Kalishwa Sumu? Jibu Lipo Hapa

October 09 2015 kuna tukio lilitokea linalomhusisha kijana Benedicto Ngonyani ambaye alituhumiwa kusambaza ujumbe ambao ulichukuliwa kama ni uzushi na kinyume cha sheria ya makosa ya mtandao.

Ujumbe huo ambao ulisambaa kwenye mitandao ya kijamii ulikuwa ukisema kwamba Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Luteni Jenerali Davis Mwamunyange amepewa sumu, suala hili lilipelekea kijana huyo kukamatwa na kupelekwa rumande.

Tumezungumza na wakili wa Benedict Ngonyani, Edward Kikuri ambaye ameeleza kesi hiyo ilipofikia hadi sasa ………
>>>’kesi imesimama kisutu kwa sababu jalada halipo, lipo Mahakama Kuu na sisi mawakili wa upande wa utetezi hatujapata wito wowote wa kuendelea na rufani hiyo isipokuwa mawakili wa serikali huwa wanaiambia mahakama kwamba kesi ya rufani au ya kupinga kupewa rufani ipo tayari mahakama kuu‘
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment