Mvua ya Dar Zilivyompeleka RC MAKONDA Jangwani Leo

Dar es salaam imekuwa moja ya majiji yanayosumbuliwa na kero za mafuriko haswa katika kipindi cha mvua, ni siku kadhaatu baadhi ya watu walilazimika kuhamishwa katika maeneo yao ya makazi kwa kukwepa miundombinu mibovu.

Leo April 16 2016 mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda alilazimika kufunga safari kuelekea katika baadhi ya maeneo kujionea hali ilivyo baada ya mvua kuharibu miundombinu

‘Kama mnavyoona,leo tumepita katika baadhi ya maeneo ikiwa ni pamoja na hapa Jangwani na kukuta hali si shwari, mitaro hii imeziba eidha kwa uchafu baada ya watu kutupa taka katika mitaro, lakini jambo la pili ni watu kujenga kwenye mikondo ya maji ’ ;-Paul Makonda

‘Kuna maeneo yamejengwa bila kuzingatia namna ya kupitisha maji, jambo ambalo linasababisha pia kuwa na ukwamishaji wa maji.’ ;-Paul Makonda

‘Ningewaomba wananchi kujiadhari kukaa kwenye mazingira hatarishi, pia kwa serikali ni kuhakikisha watu wanaotoa vibali kuangalia kutoa vibali katika maeneo yenye vikondo ya maji’
‘Natoa pole kwa watu ambao maji yameingia majumbani kwao, lakini pia tusiendelee kukaa katika mazingira hatarishi na tuangalie maeneo ambayo ni salama kwetu’ ;-Paul Makonda

Mkuu wa mkoa Paul Makonda akionyeshwa maji yalivyosambaa



Wananchi wakizungumza na mkuu wa mkoa Paul Makonda








TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment