Mwenyekiti wa Zamani CHADEMA Mwanza, Ahamia CCM

Aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Demokrsaia na Maendeleo Chedema mkoa wa Mwanza Andrian Tizeba, leo amejiunga rasmi na CCM wilayani Sengerema tawi la Lugata.

Tizeba ambaye alitangaza kujivua uanachama wa chadema Machi 29 mwaka huu baada ya kusimamishwa uongozi kwa muda wa mwaka mmoja, na kutangaza kuachana na siasa, amekabidhiwa kadi hiyo na katibu wa tawi hilo Alfred Mwambala.

Akizungumza kwa njia ya simu, Tizeba amesema uamuzi wake si wa kulazimishwa na mtu bali, ameona ni vema arudi kwenye chama chake cha awali.

Tizeba ambaye ni kaka wa mbunge wa jimbo la Buchosa, Charles Tizeba amesema, nia na dhumuni la kujiunga na chama hicho ni kutokana na utendaji wa Rais John Magufuli anaoufanya.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment