Watu 120 Wauawa Kwa Bomu Iraq

Serikali ya Iraq imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia maafa yaliyotokwea kutokana na shambulio la bomu ambalo limeua watu wapatao mia 120 katika Mji Mkuu wa nchi hiyo, Baghadad.
Katika shambujlio hilo watu 150 walijeruhiwa vibaya wakati lori lililokuwa na milipuko lilipolipuka nyakati za usiku karibu na msikiti katika wilaya ya Karanda. 

Mlipuko huo uliotokea katika eneo lenye shughuli nyingi ambapo baadhi ya watu walikkuwa wakijipatia mahitaji kwa ajili ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Tayari wapiginaji wa Islamic State wamekiri kuhusika na mlipuko huo.Muda mfupi baada ya mlipuko huo Mkuu wa majeshi ya nchi hiyo Major Generali Kadimu Shabaani alifika katika eneo la tukio.”
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment