Mapema mwezi huu, Magesa Mulongo aliwasimamisha kazi madaktari 3, manesi 6, na wafanyakazi wengine 2 wa hospitali ya Butimba kwa madai mbalimbali, yakihusisha kifo cha watoto mapacha. Lakini Mulongo alijitetea maamuzi yake kuwasimamisha, akisema ilitokana na tendo walilofanya kutoendana na sheria za kazi.
Mwenyekiti wa kamati Raphael Chegeni, alisema kamati iligundua kwamba kulikuwa na matumizi mabaya ya madaraka katika maamuzi ya mkuu wa mkoa. Na kwamba mkuu wa mkoa hakuomba taarifa ya utenda kazi ili kutambua matatizo ya hospitali.
Mmoja wa wanakamati Mhe. Zitto Kabwe ndiye aliuliza ni kitu gani hasa kilichosababisha mkuu wa mkoa kusimamisha watumishi hao, kwani kuna wagonjwa wengi wanaofariki katika hospitali husika kwa kukosa tiba na wengine wakiwa na shida mbalimbali.
Raphael Chegeni alisema mkuu wa mkoa hakufuata kanuni, zinazohitaji watumishi wa afya kusimamishwa na mabaraza yao.
"Kamati imejiridhisha kwamba mkuu wa mkoa aliwasimamisha wafanyakazi hawa wa afya kwa kutumia nguvu ya kisiasa" alisema Raphael Chegeni. Pia alionya wanasiasa, kuchanganya siasa na utoaji wa huduma za afya, hususani maeneo ya vijijini, kwani mwisho wa siku itawaamiza wakaazi wa vijijini.
Akichangia, mbunge wa viti maalumu, Mhe. Suzan Lyimo alisema viongozi wa serikali wanapaswa kutambua mchango wa watumishi wa afya wanaofanya kazi kubwa kuokoa maisha.
Kamati pia ilishauri wizara kuboresha mazingira ya kazi ya wafanyakazi wa afya, ikiwa ni pamoja na kuboresha mishahara na marupurupu.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment