Memphis DEPAY Anaondoka MAN United? Maamuzi Yake Haya Yanawashangaza Wengi


Winga mshambuliaji wa klabu ya Man United ya Uingereza Memphis Depay jina lake limeingia kwenye headlines tena, baada ya kufanya kitendo ambacho huenda kikawa na maana ya kuashiria yeye kuondoka au kukosa furaha ndani ya Man United.

Memphis amewashangaza wengi hususani mashabiki wake wa Man United wanaomfollow katika account yake ya Instagram, baada ya kuona winga huyo kaamua kufuta picha zote katika Instagram yake zinazohusu Man United ambazo aliwahi kupost na kubakisha moja akiwa na mpenzi wake pekee.

Memphis katika account yake ya Instagram amefollow watu 11 pamoja na account ya Man United pekee, kati ya hao hakuna mchezaji mwenzake wa Man United aliyemfollow, kitu ambacho kimeandikwa na mitandao mingi ya Ulaya kuwa huenda winga huyo anataka kuondoka Man United.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment