Mfumuko wa Bei wa Taifa Kwa Mwezi Februari 2016 Wapungua Kwa Asilimia 5.6

Mfumuko wa bei wa Taifa kwa Februari, umepungua kutoka asilimia 6.5 za Januari hadi 5.6 kutokana na kupungua kwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa za vyakula, matunda, mafuta ya dizeli, vinywaji na samaki.

Hata hivyo, akitangaza takwimu hizo jana, Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo alisema; “hii inamaanisha kwamba kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na ununuzi kwa mwaka ulioishia Februari ndiyo imepungua wala siyo kushuka kwa bei. Naomba lieleweke hapo. Mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa Februari umepungua kutoka asilimia 10.7 ya Januari hadi 9.5 Februari,” alisema.

Kwesigabo alisema kupungua kwa mfumuko huo kumechagizwa na kupungua zaidi kwa bei za baadhi ya bidhaa ya vyakula na zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia Februari.
Alitaja mwenendo wa baadhi ya bei za bidhaa zilizoonyesha kupungua kuwa ni gesi asilimia 10.3, dizeli asilimia 4.5 na matunda asilimia 7.2.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment