Halmashauri
 ya Jiji la Tanga ipo hatarini kuvunjwa kufuatia madiwani wake kushindwa
 kuelewana katika kikao kilichositishwa leo na Mkurugenzi mtendaji.
Kikao
 hicho cha baraza la madiwani wa Halmashairi ya Jiji la Tanga kwa mujibu
 wa barua za mwaliko walizopewa madiwani hao kilikuwa ni cha mwendelezo 
wa mkutano wa desemba 19 mwaka jana ambacho pia kilivunjika baada ya 
kutokea vurugu.
Chanzo
 cha kuvunjika kikao cha leo ni baada ya diwani wa kata ya Tangasisi 
(CUF) ambaye pia ni Naibu Meya, Mohamed Haniu kuchukua kipaza sauti na 
kutangaza kwamba kama wanataka kikao hicho kiendelee ni lazima ufanyike 
uchaguzi wa Meya.
“Kwenye
 wito wa barua za kikao hiki hakuna ajenda ya uchaguzi kwa hivyo 
tukubaliane  kwanza kwamba tunaanza na uchaguzi wa Meya ndipo tuendelee 
kwa sababu hatuna meya hadi sasa”alisema Haniu.
Tangazo
 hilo lilisababisha madiwani wa kutoka chama cha wananchi (CUF) 
kushangilia jambo lililomlazimu Meya wa Jiji, Mohamed Mustapha 
(Selebosi) kutamka kwamba kikao anakiahirisha.
Tamko la Selebosi lilisababisha madiwani wa CUF kushangilia kwa mara ya pili huku wakiimba nyimbo za kukisifu chama hicho.
Baada
 ya kuahirishwa kwa kikao hicho,Meya wa Jiji hilo, Mohamed Selebosi, 
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Abdullah Lutavi, Mbunge wa Jimbo la Tanga, 
Mussa Mbarouk na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Dk Wedson Sichalwe waliingia 
katika ofisi ya Mkurugenzi kufanya kikao chao cha ndani.
Akizungumza
 na waandishi wa habari,Kaimu Mkurugenzi , Sichalwe alisema ajenda 
ambazo zilikuwa zijadiliwe ni kuunda kamati za kudumu za halmashauri, 
kupanga ratiba za vikao vya halmashauri, kupokea taarifa ya utendaji wa 
halmashauri katika kipindi ambacho madiwani hawakuwepo na kupokea 
taarifa ya Serikali.
“Kama
 mlivyoshuhudia kikao kimevunjika,inapotokea vurugu kama vile hakuna 
sababu ya kuendelea na kikao, sheria inamruhusu  Meya kukivunja” alisema Dk Sichalwe na kusisitiza kuwa taarifa zaidi atatoa baadaye.
Diwani
 wa Kata ya Duga (CUF), Halid Rashid alisema watakuwa tayari kuendelea 
na kikao iwapo madiwani wa CCM watakubali uchaguzi wa nafasi ya meya 
ufanyike upya kwa sababu hawamtambui Mohamed Mustafa kama Meya.
“Ni
 bora Halmashauri ya jiji ivunjwe kama Serikali inalazimisha tumtambue 
Selebosi kuwa ni Meya, sisi hatutakubali akae mbele kuongoza kikao aje 
huku ndiyo kikao kiendelee” alisema Halid.
Mohamed
 Haniu (CUF) alisema anaamini Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela 
anaweza kumaliza mgogoro wa nafasi ya Meya wa Tanga kwa kutumia busara 
ya kuamuru uchaguzi wa meya ufanyike upya.
Diwani
 wa kata ya Chumbageni (CCM) Saida Gaddafi aliwataka madiwani kutoka 
chama cha CUF kukubali matokeo yaliyomtangaza Selebosi kuwa Meya kwa 
sababu hata wao walimkubali Mohamed Haniu kuwa Naibu Meya.
Mkuu
 wa Wilaya ya Tanga aliwahimiza madiwani wa Jiji kukubaliana ili vikao 
vya kupitisha miradi ya maendeleo ya wananchi viweze kuendelea.
Dalili
 za kutokea vurugu katika kikao hicho zilijitokeza mapema kufuatia jeshi
 la polisi kumshikilia Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Tanga na aliyekuwa 
mgombea wa nafasi ya Meya wa jiji la Tanga, Rashid Jumbe asubuhi kabla 
ya kuanza kikao hicho.
Taarifa
 za kushikiliwa na jeshi la Polisi diwani huyo zilienea na hata kikao 
kilipoanza hakuwepo ukumbini ambapo madiwani wenzake walisema alikamatwa
 kwa madai ya kuratibu shughuli za matangazo kuhusiana na kikao hicho 
kwa kutumia gari lililopita mitaani.
Kamanda
 wa Polisi wa Mkoa wa Tanga,Leonard Paul alithibitisha kukamatwa kwa 
diwani Rashid Jumbe na kwamba alikuwa akituhumiwa kutangaza mitaani kwa 
kutumia gari kuhusu kikao hicho.
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment