Jeshi 
 la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limefanikiwa kuwakamata watu 63
 wanaodhaniwa kuwa  majambazi wa kutumia silaha katika operesheni 
endelevu ya kuwasaka majambazi wanaofanya matukio mbalimbali.
Akizungumza
 na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Kamishna wa Polisi 
kanda maalumu Simon Sirro aamesema, miongoni mwa majambazi waliokamatwa 
ni Ibrahim Juma(31) mkazi wa Kiwalani Kigilagila, Samweli Mbonea (40) 
Fundi gereji Mkazi wa Kiwalani pamoja na Anthony Kanywenywe (60) 
Mwindaji na mkazi wa Kiwalani.
Amesema
 majambazi hao walikutwa na taa kubwa nne za magari, pawa windo moja na 
nati za magari na watuhumiwa sita  kati ya waliokamatwa wamekiri 
kushiriki katika matukio ya unyanganyi wa kutumia silaha katika maeneo 
mbalimbali likiwemo la Riki Hill Hotel katikati ya jiji na Lake oil 
Buguruni.
Katika
 tukio jingine  kikosi maalumu cha kupambana na majambazi kimefanikiwa 
kukamata silaha sita  aina ya SMG  moja ,Short gun pump action tatu na 
Rifle mbili katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
Amesema
 silaha aina ya SMG iliyokatwa kitako ilipatikana baada ya askari 
kuwafyatulia risasi majambazi hao waliokuwa eneo la vingunguti ndipo 
walipoitupa silaha hiyo ikiwa kwenye mfuko mweusi wa plastiki na wao 
kukimbia katika bonde la Mto Msimbazi.
“Tunaendelea
 kuwatafuta watuhumiwa hao na upelelezi unaendelea ili kubaini mmiliki 
halali wa silaha hiyo. Hatupotayari kuendelea kuona maovu yakiendelea 
kufanyika, jeshi lipo imara na tutapambana nao,” alisema Sirro.
Ameongeza
 kuwa jeshi hilo pia lilifanikiwa kukamata silaha Rifle mbili katika 
eneo la Masaki ambazo zilikuwa zimefichwa na kufunikwa kwa taulo zikiwa 
na maandishi ya Collessium Fitness Club  moja ikiwa na namba A 6777013 
iliyosajiliwa nchini kwa namba TZCAR 58596, na nyingine ikiwa na namba L
 691848176 iliyosajiliwa kwa namba TZCAR 75062.
Wakati
 huo huo Jeshi la Polisi Kanda maalum Dar es salaam limefanikiwa 
kukamata jumla ya risasi 15 za silaha ndogo aina ya bastola zikiwa 
kwenye magazine.
Risasi hizo alikutwa nazo mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Mamboleo Willium (41) Mfanyabiashara mkazi wa Mikocheni.
Katika
 mahojiano mtuhumiwa huyo alikiri kuwa na risasi hizo kinyume na sheria 
na kushindwa kueleza mahali alipozipata, mtuhumiwa anaendelea 
kushikiliwa  na uchunguzi unaendelea kufanyika 
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]
 
 
 
 
 
 

0 comments:
Post a Comment