DK SHEIN APONGEZWA KWA KUTEUA WAPINZANI KUWA MAWAZIRI

KLABU ya Viongozi wa Vyama vya Siasa nchini imefurahishwa na uamuzi wa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kwa hatua yake ya kuwateua wawakilishi kutoka vyama vya upinzani, huku ikielezwa ni hatua za kuigwa na viongozi wote wa Afrika.
Vyama tisa kupitia klabu ya viongozi vilivyompongeza Dk Shein ni ADA-TADEA, United Peoples Democratic Party (UPDP), Chausta na Sauti ya Umma (SAU). Vingine ni Chama cha Wakulima (AFP) na Chama cha Kijamii (CCK).Akizungumza kwenye hafla hiyo kwa niaba ya vyama vingine, Mwenyekiti wa Chama cha UPDP, Fahmi Dovutwa alisema Rais Shein amejitahidi kufanya demokrasia ionekane kuchukua mkondo wake.

Alisema hatua ya Dk Shein kuteua wawakilishi hao kuwa Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ni hatua ya kuigwa na kupongezwa kwani ameonesha ukomavu wa kidemokrasia.
“Kwanza tunampongeza Dk Shein kwa ushindi wa tetemeko aliopata…lakini kubwa ni kumpongeza kwa hatua yake ya kuteua wawakilishi na baadaye kuwa mawaziri katika vyama ambavyo havikuwa na uwakilishi, ameonesha kuwa inawezekana,” alisema Dovutwa.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment