Wizara
 ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inapenda kutaarifu Umma kuwa Daraja 
la kigamboni litaanza kutumika siku ya Jumamosi tarehe 16, Aprili, 2016 
kuanzia saa 12:00 asubuhi.
Katika
 siku za mwanzo, magari yatapita bila kulipia tozo hadi Serikali 
itakapokamilisha taratibu na kutangaza utaratibu wa kulipia. 
Aidha,
 watembea kwa miguu na waendesha baiskeli watavuka bure katika Daraja la
 Kigamboni.  Hata hivyo maguta na mikokoteni haitaruhusiwa kutumia 
daraja hilo kutokana na sababu za kiusalama.
Magari
 yatakayoruhusiwa kupita katika Daraja la Kigamboni katika siku hizo za 
mwanzo ni yale yenye uzito usiozidi tani 10, hatua ambayo itasaidia 
kufuatilia mwenendo wa upitaji wa magari katika daraja, barabara za juu 
(Interchange) katika eneo la Kurasini, pamoja na kuhakikisha kwamba 
magari yanayotoka au kuingia katika daraja hayasababishi msongamano wa 
magari katika Barabara ya Nelson Mandela, Barabara ya Kilwa na maeneo 
mengine ya jiji.  
Baada ya utaratibu kukamilika magari ya aina zote yenye uzito unaoruhusiwa kisheria yataruhusiwa kupita katika daraja.
Mambo muhimu ambayo madereva na watumiaji wengine wa barabara wanatakiwa kuzingatia ni:-
1)
 Kuzingatia sheria ya Usalama Barabarani ikiwa ni pamoja na kufuata 
mwendo kasi unaotakiwa ili kuepuka ajali na kuepuka uharibifu 
miundombinu ya daraja
2) Kufuata alama za barabarani zilizowekwa katika ‘Interchange’ ya Kurasini ili kwenda kwenye uelekeo sahihi.
3)
 Kuzingatia alama zilizowekwa kwenye milango (Toll Gates) ya Kituo cha 
kulipia tozo (Toll Plaza) ili kuepuka uharibifu wa miundombinu ya kituo 
hicho.
4)
 Madereva na watumiaji wa barabara wengine watakaosababisha uharibifu wa
 aina yeyote wa miundombinu ya daraja watatozwa faini au kuchukuliwa 
hatua nyingine za kisheria.
5) Kutunza mazingira kwa kuepuka kutupa takataka katika eneo la daraja.
Aidha,
 Wizaraya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inawataka madereva wa magari 
ya mizigo wanaoegesha katika barabara ya Nelson Mandela wakisubiri 
kuingia bandarini watafute eneo stahiki la maegesho na kuyaondoa magari 
hayo kwani hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaoenda kinyume 
na agizo hili.
Msongamano wa magari hayo husababisha uharibifu wa barabara na usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara katika eneo hilo.
Imetolewa na;
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu  (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
14 Aprili, 2016
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment