Paul MAKONDA Katoa Siku Sita, Haya Mambo Matatu Yashughulikiwe Jijini Dar

April 12 2016, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda ametoa maagizo kwenye mambo matatu wakiwemo ombaomba wa mabarabarani, majengo makubwa yaliyojengwa kinyume na taratibu pasipo kuwa na parking na wamiliki wa bar kupiga muziki nje ya utaratibu wa vibali vyao. 

Paul Makonda ametoa siku sita mpaka April 18 ombaomba ndani ya Dar es salaam kuondoka mabarabarani, wamiliki wa majengo walipe faini na kuweka utaratibu wa magari yatapark wapi au kubomoa majengo yao, na kuhusu wamiliki wa Bar Paul Makonda  ameyazungumza haya……
>>>’wamiliki wa bar wanaowapigia watu kelele wafuate sheria walizopewa kama ni mwisho saa sita kupiga muziki iwe hivyo na muziki huo upigwe kwenye maeneo husika, mtu ambaye anapiga muziki nje ya utaratibu wa kibali chake maana yake ajiandae kunyang’anywa leseni na kufutiwa kibali chake na faini hiyo atailipa mwenyewe’:-Paul Makonda
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment