April 12 2016, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda
 ametoa maagizo kwenye mambo matatu wakiwemo ombaomba wa mabarabarani, 
majengo makubwa yaliyojengwa kinyume na taratibu pasipo kuwa na parking 
na wamiliki wa bar kupiga muziki nje ya utaratibu wa vibali vyao. 
Paul 
Makonda ametoa siku sita mpaka April 18 ombaomba ndani ya Dar es salaam 
kuondoka mabarabarani, wamiliki wa majengo walipe faini na kuweka 
utaratibu wa magari yatapark wapi au kubomoa majengo yao, na kuhusu 
wamiliki wa Bar Paul Makonda  ameyazungumza haya……
>>>’wamiliki wa bar wanaowapigia watu kelele wafuate sheria walizopewa kama
 ni mwisho saa sita kupiga muziki iwe hivyo na muziki huo upigwe kwenye 
maeneo husika, mtu ambaye anapiga muziki nje ya utaratibu wa kibali 
chake maana yake ajiandae kunyang’anywa leseni na kufutiwa kibali chake 
na faini hiyo atailipa mwenyewe’:-Paul Makonda 
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]
0 comments:
Post a Comment