Bunge 
 linaanza rasmi usajili wa wabunge na watumishi wa Bunge hilo pamoja na 
wageni mbalimbali, wanaoingia bungeni kwa kutumia mfumo wa kisasa wa 
kuchukua alama za vidole.
Sambamba
 na mfumo huo, Bunge pia limetoa taarifa rasmi ya kudhibiti urushaji wa 
matangazo ya Bunge ambayo sasa vyombo vya habari vya kielektroniki 
havitaruhusiwa kuingia ndani ya ukumbi wa bunge na kamera kwa lengo la 
kurekodi yanayoendelea.
Na
 badala yake, jukumu la kurusha matangazo ya vikao vya Bunge litafanywa 
na Bunge lenyewe kupitia Feed Maalum ili kurahisisha kila kituo cha 
redio na televisheni kupata matangazo hayo kwa sehemu walipo bila 
kufunga mitambo yao bungeni.
Hayo
 yalibainishwa jana na Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashilillah wakati 
akitoa taarifa kwa Naibu Spika wa Bunge hilo, Dk Tulia Ackson alipofanya
 ukaguzi wa ukarabati uliofanywa ndani ya Ukumbi wa Bunge linaloanza 
vikao vyake vya Bajeti katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la 11 mjini hapa.
Dk
 Kashilillah alisema kuanzia jana wabunge wataanza usajili kwa njia ya 
kuchukuliwa alama za vidole badala ya utaratibu wa zamani wa kujisajili 
kwa kutumia makaratasi. 
Alisema
 usajili huo utachukua alama za vidole vyote 10 na lengo la kutumia 
mfumo huo ni kuboresha kanzi data ya Bunge na kwamba usaili huo 
utapunguza pia matumizi ya makaratasi ambayo yana gharama.
“Tumeanza
 usajili huo leo (jana) kwa wabunge waliofika, ila tutaendelea kusajili 
nadhani ndani ya wiki tutakuwa tumekamilisha kazi hiyo, na tumejipanga 
kuifanikisha kwa haraka,” alisema Dk Kashilillah.
Akizungumzia
 usajili huo, Dk Kashilillah alisema utasaidia kufahamu idadi ya wabunge
 waliohudhuria vikao vya bunge na hivyo itakuwa rahisi kwenye kazi ya 
upigaji kura wakati wa kupitisha hoja mbalimbali.
Alisema
 Bunge limeboreshwa na kuwa la kisasa zaidi ambapo kila meza ya mbunge 
ndani ya ukumbi huo, itakuwa na ‘tablet’ itakayomuwezesha kufuatilia 
majadiliano ya bunge hata ya siku zilizopita na pia wabunge wataweza 
kuona ratiba ya shughuli mbalimbali za Bunge.
Akizungumzia
 elimu kwa wabunge hao juu ya matumizi ya mfumo huo, Dk Kashilillah 
alisema wameandaa utaratibu wa kuwaelimisha wabunge hao juu ya matumizi 
ya mfumo huo, ili iwe rahisi kwao kuutumia.
Naye
 Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Bunge, Didas 
Wambura alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha matangazo ya bunge 
yanapatikana kwenye vituo vya televisheni kama ilivyopangwa.
Wambura
 alisema kuanzia sasa Bunge litarusha matangazo ya Bunge lenyewe kupitia
 feed maalumu ili kurahisisha kila kituo cha televisheni na redio kupata
 matangazo hayo kwa sehemu walipo, bila kufunga mitambo yao bungeni.
“Tutarusha matangazo ya Bunge wenyewe tutatumia Feed Maalumu itakayorushwa na satelaiti ya INTELSAT 17,” alisema Wambura.
Kutokana
 na hatua hiyo, vituo vya televisheni na redio nchini havitaruhusiwa 
kuingiza kamera zao ndani ya Ukumbi wa Bunge kurekodi vikao hivyo na 
badala yake wanapaswa kutumia Masafa ya Matangazo ya Bunge.
Katika
 mabadiliko hayo, pia idadi ya viti vipya 94 vimefungwa ndani ya Ukumbi 
wa Bunge hilo na hivyo kufanya idadi ya vitu vyote vya ukumbi kuwa 404.
Kwa
 upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano wa Bunge,
 Owen Mwandumbya alisema watakaa na wadau wote wa habari ili kuona ni 
namna gani wataweza kupata matangazo hayo.
“Haturuhusu
 wapiga picha za televisheni na redio kuingia na kamera ndani ya Ukumbi 
wa Bunge kurekodi, kazi hiyo itafanywa na Bunge, ila waandishi wa habari
 wa magazeti na wapigapicha za mnato wataendelea kuingia,” alisisitiza Mwandumbya.
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment