Upande
 wa Mashitaka katika kesi ya Josephat Gwajima, Askafu wa Mkuu wa Kanisa 
la Ufufuo umekataa kuendelea kupeleka mashahidi wake katika Mahahaka ya 
Hakimu Mkazi Kisutu kwa madai ya kutaka kesi isimamishwe ili isikilizwe 
rufaa yao.
Upande
 wa mashitaka ulipeleka mahakamani hapo notisi ya rufani tarehe 25 
Aprili mwaka huu, kupinga kutopokelewa kwa ushahidi wao wa CD na picha 
zilizopelekwa mahakamani hapo.
Shadrack
 Kimaro, Mwanasheria Mwandamizi wa Serikali aliiomba mahakama kuwa, kesi
 hiyo isimamishwe mpaka utakapotolewa uamuzi wa rufaa ya kupinga 
kukataliwa kwa ushahdi wa CD na picha zilizofikishwa mahakamani hapo 
kama kielelezo cha kesi hiyo.
Shadrack
 amesema kuwa, ushahidi huo ulioambatana na ripoti ya mtaalamu wa picha 
na barua ya ZCO iliyokwenda kwa mtaalamu wa picha, vyote vilikataliwa 
mahakamani hapo.
Hata
 hivyo, upande wa mshtakiwa uliomba mahakama kufuta kesi hiyo kutokana 
na upande wa mashitaka kukosa ushahidi na kwamba kesi haiwezi 
kusimamishwa kutokana na kungojaa rufaa iliyokuwa bado haijafunguliwa.
Cyprian
 Mkeha, Hakimu Mfawidhi baada ya kusikiliza pande zote mbili amesema 
kuwa, kesi hiyo itatajwa tena tarehe 2 Juni mwaka huu.
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]
0 comments:
Post a Comment