
FIFA imeagiza Simba katika barua yake iliyoandikwa May 3 2016 na kufika Tanzania leo May 6 2016 kumlipa Musoti Tsh milion 64.2 za kitanzania pamoja na gharama ya kikao cha Idara ya Utatuzi wa Migogoro (Desputes Resolution Chamber) cha FIFA.

Donald Musoti
Miongoni mwa fedha wanazotakiwa kulipa Simba ni Tsh 4,582,000 za fidia, Tsh 1,145,500 ya gharama za kikao cha idara ya migogoro ya FIFA, Musoti aliyesajiliwa na Simba msimu wa 2014/15 na kuachwa alilalamika FIFA kwa kumtumia mwanasheria wake Felix Majani, FIFA ambayo iliona Musoti ana hoja, hivyo Simba imetakiwa kumlipa.
Kiasi kingine anachodai ni Dola 600 (Sh 1,290,000) zilizobaki katika usajili ambapo jumla yake ni Sh 64.2 milioni. Pia Mosoti anamlipa Mwanasheria wake dola 2,000 (Sh 4.3 milioni) kwa ajili ya kusimamia kesi hiyo. Kama Simba itashindwa kulipa deni hilo ndani ya siku 30, itaponywa point tatu au kushushwa daraja.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]
0 comments:
Post a Comment