Utafiti wa Twaweza: Asimilia 96 wanakubali Utendaji wa Rais MAGUFULI

Utafiti uliofanywa na shirika la Twaweza, umebaini kuwa asilimia 96 ya Watanzania wanakubali utendaji wa Rais Dkt John Pombe Magufuli.
Utafiti huo uliopewa jina ‘Rais wa Watu’ ulijikita katika tathmini na matarajio kwa wananchi kwa rais huyo wa awamu ya tano.

“Watu wanakubali hatua zinazochukuliwa na uongozi wa awamu ya tano wa rais John Pombe Magufuli, hususan katika kuondoa wafanyakazi hewa, sera ya elimu bure, na uhamasishaji wa wafanyakazi wa watumishi wa serikali kutokana na makosa mbalimbali,” alisema Mkurugenzi wa Twaweza, Aidan Eyakuse.
Jumla ya watu 1,813 kutoka Tanzania bara (Zanzibar haihusiki katika utafiti huu) walihojiwa kwenye utafiti huo kati ya tarehe 4 Juni na tarehe 20 Juni.

Miongoni mwa vitu alivyoahidi Rais Magufuli ni wanafunzi kusoma bure akiwa mastari wa mbele kupinga vitendo vya rushwa.
BY: EMMY MWAIPOPO
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment