TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Makamu
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania SAMIA SULUHU HASSAN 
ameviagiza viwanda vyote nchini kutumia msibomilia (BARCODES) za 
Tanzania kama hatua ya kuimarisha masoko na utambulisho wa bidhaa za 
Tanzania katika masoko ya ndani na ya nje ya nchini.
Makamu
 wa Rais ametoa agizo hilo kwenye uzinduzi wa kampeni ya “NUNUA 620 
Nunua Bidhaa za Tanzania” pamoja na Kusherekea miaka MITANO ya Taasisi 
ya Global Standard One –GSI-kwenye Viwanja wa Mwalimu Nyerere katika 
Maonyesho ya  40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es salaam (SABASABA) 
mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonyesho.
Makamu
 wa Rais amesema matumizi ya BARCODES ni muhimu na ni ya lazima kwa 
sababu yanajumuisha taarifa nyingi ikiwemo asili ya bidhaa,jina la 
kampuni, kumbukumbu za uzalishaji,utunzaji,usafirishaji na usambazaji wa
 bidhaa.
Ameleeza
 kwamba itakuwa ni aibu kubwa kama katika masoko ya ndani ya nchi bado 
kutakuwa na bidhaa zinazotumia msibomilia (BARCODES) za nje na  
kusisitiza kuwa matumizi ya Barcodes za Tanzania zitazuia na kupungua 
upotevu wa ajira kwa wataalamu wa ndani ya nchi.
Makamu
 wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN amesema kuwa serikali ya awamu ya TANO ipo 
Tayari kufanya kazi na sekta binafsi katika kuleta mapinduzi makubwa 
yatakayosaidia kukuza uchumi wa taifa.
Kuhusu
 uanzishwaji wa Majukwa ya kumwezesha wanawake Kiuchumi  nchini, Makamu 
wa Rais amesema kuwa atahakikisha majukwaa hayo yanaleta matokeo chanya 
na yenye tija kwa wanawake Wakitanzania mijini na viijijini kwa 
kuwezeshwa kupata kupata elimu ya ujasiriamali,fursa za 
masoko,upatikanaji wa mikopo nafuu pamoja na elimu ya kukabiliana na 
changamoto mbalimbali zinazowakwaza wanawake kiuchumi.
Makamu
 wa Rais pia ametoa wito maalum kwa wanawake kote nchini kujiunga na 
majukwaa hayo pindi yatakapoanzishwa kwenye maeneo yao kwa sababu 
yatakuwa na faida kubwa kwao kwa kuunganisha nguvukazi zao na kuzalisha 
bidhaa zenye ubora wa hali ya juu.
Imetolewa na
Ofisi ya Makumu wa Rais
2-Jul-16
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment