Serikali
   imejiandaa kuleta Muswada wa Sheria bungeni kutoa haki ya kusoma kwa 
watoto wote wa kike na kiume wa shule za msingi, sekondari na 
kutoruhusiwa kuoa au kuolewa.
Aidha,
 Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema serikali 
inaendelea kukamilisha utaratibu wa kupata maoni ya wananchi kuhusu 
marekebisho ya Sheria ya Ndoa na kutungwa kwa Sheria mpya ya Mirathi na 
Urithi kuondokana na mkanganyiko uliopo kuhusu sheria hiyo.
Bunge
 lilielezwa hayo jana mjini Dodoma wakati waziri huyo akijibu swali la 
nyongeza la Mbunge wa Ileje, Janeth Mbene (CCM) aliyehoji ni lini 
serikali itaanza maandalizi ya kuchukua maoni juu ya kufanya marekebisho
 sheria ya ndoa ya mwaka 1971.
Akijibu
 swali hilo, Dk Mwakyembe alisema hatua za awali zimeshaanza kuchukuliwa
 na wizara hiyo ili kupata maoni ya wananchi juu ya marekebisho ya 
sheria hiyo ya ndoa ya mwaka 1971 na kutungwa kwa sheria mpya ya mirathi
 na urithi.
Alisema
 serikali ina nia ya dhati ya kufanyia marekebisho sheria ya ndoa na 
kwamba mchakato huo ulisitishwa kwa kuwa Tume ya mabadiliko ya Katiba 
ilikuwa ikikusanya maoni kuhusu mabadiliko ya katiba , hivyo walidhani 
wananchi wangetoa pia maoni juu ya sheria hiyo.
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment