Tanzania imewapokea wafanyabiashara 50 kutoka Urusi kuja kuwekeza kwenye sekta mbalimbali nchini. 
Akieleza
 ujio wa wafanyabiashara hao, Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji wa 
Wizara ya Viwanda na Biashara, Adolf Mkenda alisema baada ya 
kushirikiana kisiasa kwa muda mrefu, Urusi imeamua kuisaidia Tanzania 
kuimarisha uchumi wake. 
Wafanyabiashara hao wanatarajia kukutana
 leo katika kongamano litakalobainisha fursa zilizopo kwa wageni hao 
kuwekeza hasa kwenye kilimo, nishati, usafiri, viwanda na madini. 
Urusi
 ni miongoni mwa mataifa 10 makubwa kiuchumi duniani na imeendelea 
kisayansi na kiteknolojia huku ikiwa na idadi kubwa ya watu. 
Rais
 mstaafu, Jakaya Kikwete wakati akiwaaga mabalozi 36 wa Tanzania, 
aliwaagiza kulitangaza Taifa huko waliko ili kuvutia wawekezaji na 
kuwaongezea masoko Watanzania. 
Balozi wa Tanzania nchini Urusi, 
Wynjones Kisamba ameanza kuonyesha njia kwa ugeni huo unaotarajia 
kuongeza biashara za Taifa hilo. 
Mkurugenzi wa Kituo cha 
Uwekezaji nchini (TIC), Julieth Kairuki alisema Watanzania wana uhakika 
na soko la mbogamboga, matunda, asali na bidhaa nyingine nchini humo na 
kwamba kinachotakiwa ni kuongeza ubora ili kukidhi viwango vya 
kimataifa. 
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment