Serikali 
 imesema itawafukuza kazi maofisa wa Serikali ambao wanaweka vikwazo na 
kuwakwamisha waandishi wa habari kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa 
kupata habari na taarifa mbalimbali kutoka serikalini.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye aliyasema hayo 
jijini Mwanza wakati alipozungumza na wadau wa utamaduni, habari na 
michezo kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza.
Alisema
 hayo wakati akitoa ufafanuzi wa swali lililoulizwa na Mwandishi wa 
Habari wa ITV/ Radio One anayefanyia kazi zake mikoa ya Kanda ya Ziwa, 
Cosmas Makongo ambaye alitaka apate msimamo wa Serikali juu ya hatua 
zitakazochukuliwa na serikali kutokana na wimbi la unyanyasaji wa 
kijinsia unaofanywa na baadhi ya watendaji wa Serikali kwa waandishi wa 
habari nchini.
Makongo
 alisema akiwa wilayani Chato mkoani Geita hivi karibuni alizuiliwa 
kuandika habari na ofisa mmoja wa Serikali hadi pale atakapopata kibali 
kutoka kwa Mkuu wa Wilaya.
“Kumeibuka
 wimbi la unyanyasaji wa kijinsia kwa waandishi wa habari, ukifika Chato
 huandiki habari mpaka upate kibali kutoka kwa Mkuu wa Wilaya, 
nilizuiliwa kuandika habari hivi karibuni wakati nafanya habari ya 
uchunguzi wa mabilioni ya fedha wilayani humo,” alisema Makongo na kuhoji,
 “Mheshimiwa Waziri tukiendelea kusubiri vibali kutoka kwa watawala je, tutafichua maovu?” 
Nape
 alisema kuwa msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John 
Magufuli ni kuvitumia vyombo vya habari katika kufichua maovu 
yanayofanywa na baadhi ya watu katika jamii. 
“Kama
 kuna Ofisa wa Serikali anaweka kizuizi kwa mwandishi wa habari ili 
asipate habari na kushindwa kutimiza wajibu wake tutamfukuza kazi,” alisema Nape.
Aliwataka
 maofisa wa habari kote nchini wawe tayari kutoa taarifa mbalimbali za 
maendeleo zilizopo kwenye maeneo yao kwa wakati ili waandishi 
wauhabarishe umma.
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment