Kwa
 kutumia kifaa hicho, dereva atakuwa na uwezo wa kuzima pikipiki au gari
 kwa kutumia simu ya mkononi, ambayo namba yake itakuwa imefungwa katika
 chombo hicho cha usafiri.
Akizungumzia
 kifaa hicho, Mwalimu wa Teknolojia ya Mawasiliano wa Veta, Valerian 
Sanga alisema alishirikiana na mwalimu mwenzake wa chuo hicho 
anayefundisha masuala ya umeme, Christian Brighton kubuni kifaa hicho 
kilichowachukua miaka miwili kukamilika.
“Wiki
 tatu zilizopita ndio tumekamilisha kifaa hiki na kuanza kufanya kazi, 
tukafunga kwenye pikipiki hii (akionesha) kupima na kuonesha watu namna 
ya kuweka ulinzi kwenye vifaa vyao kwa kuwa mifumo kama hii, inauzwa 
katika kampuni za nje lakini ni gharama sana,” alisema.
Mwalimu huyo anatoka Kituo cha Veta Kipawa jijini Dar es Salaam, ambacho kilibuni mfumo huo ili kudhibiti wizi wa pikipiki.
Ubunifu
 huo ulichangia mamlaka hiyo, kupata tuzo ya mshindi wa jumla wa 
Maonesho ya Kimataifa ya 40 Dar es Salaam, yanayoendelea katika viwanja 
vya Mwalimu Julius Nyerere. 
Sanga alisema kifaa hicho kina GPS na kinatumia mawasiliano ya simu kwa kutumia GSM, itakayo saidia kujua sehemu pikipiki au gari lilipo, lakini pia kikimwezesha mmiliki kuzima na kuwasha usafiri wake popote ulipo.
Sanga alisema kifaa hicho kina GPS na kinatumia mawasiliano ya simu kwa kutumia GSM, itakayo saidia kujua sehemu pikipiki au gari lilipo, lakini pia kikimwezesha mmiliki kuzima na kuwasha usafiri wake popote ulipo.
“Unatumia
 simu ya mkononi ambayo namba zako zinakuwa zimefungwa katika chombo cha
 usafiri, ili zikuwezeshe kuzima kama kimeibiwa ambapo baada ya dakika 
tano kitazima na hakitawaka mpaka utume tena ujumbe wa kutaka iwake,” alisema.
Sanga
 alisema kwa sasa wanafunga kifaa hicho kwa gharama ya Sh 400,000, 
lakini anatarajia baadaye watakapopata oda nyingi, watapunguza bei kwani
 kwa siku nne tangu kuanza maonesho hayo wameshapata watu wengi 
wanaohitaji.
“Tunategemea
 kupata watu wengi wanohitaji na tayari watu wawili; mmoja ana pikipiki 
ishirini na mwingine kumi, wametaka tuwafungie huku tukiamini mpaka 
maonesho yaishe tutapata wengi zaidi,”alisema.
Alisema
 ili kukidhi mahitaji hayo, wamekuwa wakifundisha wanafunzi wa chuo 
hicho ili washirikiane katika kutengeneza vifaa hivyo kwa wingi ikiwa 
watajitokeza wengi wanaozihitaji.
Baadhi
 ya watu waliotembelea kuona pikipiki hiyo, walishangazwa na utaalamu 
huo kufanyika nchini na kutaka serikali kusaidia, hususani wakati huu wa
 taifa linapojiandaa kwa uchumi wa viwanda.
Mmoja
 wa wananchi hao, Godwin Mlulu alisema kifaa hicho kimekuja wakati 
muafaka kutokana na kukithiri kwa wizi wa pikipiki. Lakini alipendekeza 
bei ipunguzwe, kwa kuwa wamiliki wengi wa pikipiki za biashara, ni wenye
 kipato cha chini.
 TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
[MATUSI HAYARUSIWI]

0 comments:
Post a Comment