Mganga wa Zahanati Kigoma Atiwa Mbaroni kwa Tuhuma za Kumbaka Mgonjwa

Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linamshikilia Mganga wa Zahanati ya kijiji cha Kidahwe wilayani Kigoma kwa tuhuma za kumbaka mgonjwa aliyekuwa akimtibu katika zahanati ya kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ferdinand Mtui amemtaja mganga huyo kuwa ni Ibrahim Bundala (29)na kwamba anatuhumiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka 14 aliyefika katika zahanati hiyo kwa ajili ya kupata matibabu.

Amesema mtuhumiwa huyo ambaye atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika alitenda kosa hilo baada ya binti huyo kuingia katika chumba cha daktari kwa ajili ya kumueleza ugonjwa anaoumwa.

Katika tukio jingine wahamiaji 55 toka Burundi wamekamatwa katika maeneo mbalimbali baada ya kuingia nchini kinyume cha sheria na wamekabidhiwa idara ya uhamiaji kwa ajili ya taratibu nyingine ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment