DK SHEIN Tumbua Majipu Kama Rais MAGUFULI... Ni Bora Ufe Kwa Kujali Wengine Kuliko Kujinufaisha - Askofu

Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ametakiwa afuate nyayo na dhana ya utumbuaji majipu ya Rais John Magufuli kwa kuwa imegusa maisha ya wananchi wanyonge.

Wito huo ulitolewa juzi na Askofu mstaafu wa Kanisa la Anglikana, Jimbo la Tabora Francis Ntiruka katika mahubiri ya Ijumaa Kuu katika Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu mjini Dodoma.

Askofu huyo alisema Yesu Kikristo aliteseka hadi kuuawa kwa ajili ya kutetea haki za wanyonge na vivyo hivyo lazima viongozi wawatetee wanyonge.

Alisema kifo chake kiliambatana na vipigo vya mateso ya dhihaka nyingi kutoka kwa watawala waliotaka kujinufaisha wao binafsi pasipo kujali wengine.
“Ni bora ufe kwa ujali wengine kuliko kujinufaisha, alisema askofu huyo ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha St John.

Alimtaka Dk Shein aliyeapishwa juzi kuwa Rais wa Zanzibar ajipange kuhakikisha analeta umoja na amani ya Wazanzibari na kutumbua majipu kama anavyofanya Rais Magufuli.

Alisema Watanzania wana mateso mengi kama ya umaskini, magonjwa, kuporwa haki na rasilimali zao jambo alilosema bila kutafutiwa ufumbuzi, malalamiko yao hayataisha.
TUPE MAONI YAKO HAPO CHINI
[MATUSI HAYARUSIWI]
Share on Google Plus
    Facebook Comment
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment